Uingereza yasema haiungi mkono mpango wa Israel kwa Gaza
2 Aprili 2025Falconer, ameliambia bunge la nchi hiyo kwamba wana wasiwasi mkubwa kuhusu kuzuka upya kwa uhasama katika ukanda huo.
Israel yapendekeza mpango mpya wa kuachiwa mateka
Falconer ameongeza kusema kuna hatari kubwa kwa kuwa Israel inachukuwa hatua nje ya utetezi wake halali.
Israel yadaiwa kukiuka sheria ya kimataifa ya kibinadamu
Alipoulizwa kuhusu hatua ya Israel ya kuzuia misaada, Falconer alisema kuwa wamebainisha kuna hatari kubwa ya ukiukwaji wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu kutoka kwa serikali yaIsraelna kwamba wataendelea kuishinikiza kuhusu masuala hayo.
Uchunguzi kufanywa ya mauaji ya wahudumu wa afya Gaza
Wakati huo huo, Ujerumani imetoa wito wa uchunguzi baada ya wahudumu wanane wa afya kuripotiwa kuuawa katika ukanda wa Gaza.
Msemaji wa ofisi ya mambo ya nje mjini Berlin, amesema leo kuwa wanaamini uchunguzi wa kina unapaswa kufanywa kuhusu matukio hayo.