Uingereza yaandaa mkutano dhidi ya wahamiaji haramu
31 Machi 2025Matangazo
Kulingana na dondoo za hotuba ya Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer iliyoonekana kabla ya mkutano huo, biashara hiyo inatumia vibaya mianya ilioko katika taasisi zao, kugonganisha mataifa na kunufaika kutokana na kushindwa kwao kushirikiana katika ngazi ya kisiasa.
Wahamiaji haramu 600 wakamatwa Uingereza
Mkutano huo wa OIC unalenga kuangazia kila hatua ya biashara hiyo haramu ya kimataifa ya usafirishaji haramu wa watu, inayojumuisha wauzaji wa boti ndogo zinazotumika kusafirisha watuhao kutoka Ufaransa hadi Uingereza, pamoja na kampuni za teknolojia ambazo mitandao yao ya kijamii hutumika kutangaza biashara hiyo haramu.