Uingereza: Tuko tayari kuisaidia Ukraine kupata amani
25 Aprili 2025Matangazo
Reed amesema muungano thabiti wa mataifa unahitajika ili kuhakikisha kwamba makubaliano yoyote ya amani yanaweza kutekelezwa .
Mkutano wa ngazi ya juu kuhusu Ukraine wagonga mwamba
Haya yanajiri huku waziri mkuu wa Uingereza Keir Starmer akisema kuwa mazungumzo ya kujaribu kumaliza vita yamefikia kiwango cha juu na akasisitiza wito kwa Urusi kushiriki katika mazungumzo hayo na kukubali kusitisha mapigano.
Hii leo, gazeti la The Times, limeripoti kuwa huenda Uingereza ikafutilia mbali mipango ya kutuma vikosi vyake Ukraine kwasababu athari zake zinazingatiwa kuwa juu.
Gazeti hilo hata hivyo, limesema kuwa wakufunzi wa kijeshi bado watatumwa nchini Ukraine.