Uingereza mwenyeji wa mkutano 'biashara chafu' ya wahamiaji
31 Machi 2025Matangazo
Mawaziri wa mambo ya ndani kutoka Ujerumani na Ufaransa ni miongoni mwa wanaohudhuria mkutano huo wa siku mbili, unaofanyika wakati Uingereza ikikabiliana na kiwango kikubwa cha wahamiaji.
Taarifa iliyotolewa na wizara ya mambo ya ndani ya Uingereza imesema Starmer atashinikiza kupatikana kwa suluhisho la kudumu na la pamoja kuzuwia kile anachokiita "kitisho cha wahamiaji kwa usalama na ubinaadamu."
Wawakilishi kutoka Ulaya, Asia, Afrika na Amerika Kaskazini, ikiwemo Marekani, wanahudhuria mkutano unaomalizika kesho, Jumanne.