Uhalifu wa kisiasa waongezeka Ujerumani
20 Mei 2025Matangazo
Idadi hiyo ni kubwa zaidi kuwahi kurekodiwa tangu takwimu zilipokusanywa kwa mara ya kwanza mwaka 2001, huku kukiwa na ongezeko la makosa yanayohusishwa na siasa kali za mrengo wa kulia.
Kulingana na BKA, uhalifu huo umeongeza kwa takribani asilimia 40 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia.
Kati ya takwimu hizo, visa 42,788 vilikuwa vya siasa kali za mrengo wa kulia, ambayo ni karibu asilimia 50 ya uhalifu uliochochewa kisiasa, ikiwa ni ongezeko la visa 28,945 vilivyorekodiwa mwaka 2023.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ujerumani, Alexander Dobrindt, amesema ongezeko hilo linatokana na mgawanyiko uliopo katika jamii na kuongezeka kwa chuki.