Uganda yasitisha ushirikiano wake wa kijeshi na Ujerumani
26 Mei 2025Matangazo
Mkuu wa majeshi ya Uganda Jenerali Muhoozi Kainerugaba alisema wana matatizo na Balozi wa sasa wa Ujerumani nchini Uganda Matthias Schauer akisema hafai na hana sifa za kuwa nchini humo.
Kainerugaba amesisitiza kuwa kauli yake haiwalengi watu wa Ujerumani anaowaheshimu sana.
Jeshi la Uganda lamtuhumu balozi kwa Ujerumani kuunga mkono uasi
Awali jeshi la Uganda lilizishutumu baadhi ya balozi za Ulaya kuunga mkono makundi hasi na ya kisaliti ikimlenga moja kwa moja balozi Schauer.
Hii ni baada ya wanadiplomasia wa Ulaya kukosoa tabia ya mtoto wa rais wa Uganda Yoweri Museni, Muhoozi Kainerugaba.