Uganda yakanusha makubaliano na Marekani kuhusu wahamiaji
20 Agosti 2025Katika ujumbe kwa shirika la habari la Reuters, Oryem amesema kulingana na anachofahamu, hawajafikia makubaliano kama hayo.
Ikinukuu hati za ndani za serikali ya Marekani, shirika la habari la CBS liliripoti jana kuwa Marekani ilikuwa imefikia makubaliano ya kuwahamishia watu nchini Uganda pamoja na Honduras kama sehemu ya harakati zake za kuongeza kasi ya kuwafukuza wahamiaji haramu kwenda nchi ambazo hawana uraia.
Afrika Kusini yakosoa uhamisho wa wahalifu kutoka Marekani
Ripoti hiyo ya CBS imesema makubaliano hayo na Uganda pamoja na Honduras yametokana na kifungu cha sheria ya uhamiaji ya Marekani inayoruhusu waomba hifadhi kuhamishwa hadi nchi za tatu ikiwa serikali yaMarekani itabainisha mataifa hayo yanaweza kusikiliza madai yao kwa haki.