Ufaransa yasema italitambua rasmi taifa la Palestina
25 Julai 2025Macron amesema Ufaransa itafanya hivyo ifikapo mwezi Septemba, katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Uamuzi huo umeifanya Ufaransa kuwa taifa lenye ushawishi mkubwa zaidi barani Ulaya kuchukua hatua hiyo ya wazi, huku mvutano ukizidi kati ya Israel na Wapalestina.
Alisisitiza kuwa ni lazima kumaliza vita huko Gaza na kuhakikisha ustawi wa raia, sambamba na kuhakikisha taifa la Palestina lina uwezo wa kustawi kwa amani.
Tangazo la Macron limepokelewa kwa hasira na serikali ya Israel. Naibu Waziri Mkuu wa Israel Yariv Levin ameutaja uamuzi huo kuwa "wa aibu" na kusema kuwa ni "msaada wa moja kwa moja kwa ugaidi."
Naye waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio amesema Marekani inaupinga mpango wa Ufaransa kulitambua rasmia taifa la Palestina. Rubio amesema uamuzi huo wa Macron ni wa kukurupuka.