SiasaUfaransa
Ufaransa: Hatukubaliani na matamshi ya balozi wa Marekani
25 Agosti 2025Matangazo
Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa imesema kwenye taarifa jana Jumapili kwamba imemtaka Kushner kufika kwenye Wizara hiyo na kuongeza kuwa madai yake "hayakubaliki."
Taarifa hiyo imesema Ufaransa inapinga vikali madai hayo ya Kushner na kwamba mamlaka zimekuwa zikikabiliana kikamilifu na ongezeko la visa vya chuki dhidi ya Wayahudi tangu shambulizi la Oktoba 7, lililofanywa na Hamas nchini Israel.
Ikulu ya White House haijatoa tamko lolote licha ya kuombwa kuzungumzia hilo, ingawa msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje Tommy Piggot alinukuliwa jana jioni akisema anaunga mkono matamshi hayo na Kushner.