MigogoroAmerika ya Kaskazini
Trump, Zelensky na viongozi wa EU kukutana Washington
18 Agosti 2025Matangazo
Majadiliano hayo yote yanalenga kupata ufumbuzi wa mzozo kati ya Urusi na Ukraine na kuwaleta pamoja Zelenky na Rais wa Urusi Vladimir Putin katika meza ya mazungumzo. Itakumbukwa kuwa mwishoni mwa juma, Trump alikutana pia na kufanya mazungumzo na Putin huko Alaska, Marekani.
Miongoni mwa viongozi wa Ulaya watakaoshiriki mazungumzo hayo ni pamoja na Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz, Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Mark Rutte.