Trump na Modi waafikiana suala la urari wa biashara
14 Februari 2025Matangazo
Trump ametoa matamshi hayo wakati wa mkutano na waandishi habari mjini Washington akiwa pamoja na Modi anayeitembelea Marekani. Amesema kwa kuanzia, India imekubali kununua zaidi mafuta na gesi kutoka Marekani ili kupunguza pengo la thamani ya biashara kati ya mataifa hayo mawili.
Trump vilevile amesema Marekani itaongeza mauzo ya silaha kwa India kuanzia mwaka huu ikiwemo ndege za kivita chapa F-35.
Tofauti ya uzani wa biashara kati ya Marekani na mataifa mengine duniani ni mojawapo ya sababu ambazo Trump ametumia kuhalalisha hatua yake ya kuongeza ushuru kwa bidhaa kutoka nje.
Mbali ya biashara viongozi hao wawili wameafikiana pia kufanya kazi pamoja kukishinda kile wamekiita "kitisho cha ugaidi wa itikadi kali za Kiislamu".