MigogoroMarekani
Trump kuwakusainisha Mkataba wa amani Azerbaijan na Armenia
8 Agosti 2025Matangazo
Trump ameandika kwenye mtandao wa kijamii wa Truth Social kwamba wakuu hao, Waziri Mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan na Rais wa Azerbaijan, Ilham Aliyev, watahudhuria hafla ya utilianaji saini itakayofanyika kwenye Ikulu ya White House, mjini Washington.
Nchi hizo mbili zimekuwa zikifanya mazungumzo kwa lengo la kupata azimio la amani, lakini bado hakujakuwa na mafanikio.
Mahasimu hao na zilizokuwa jamhuri za Kisovieti wamepigana vita mara mbili wakizozania eneo la Karabakh.