SiasaUrusi
Trump kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na Putin
18 Machi 2025Matangazo
Katika chapisho kwenye mtandao wa kijamii hapo jana, Tump alisema kuwa masuala mengi ya makubaliano hayo ya mwisho yamekubaliwa, lakini bado yako yaliosalia.
Trump ameongeza kusema kuwa kila wiki, wanajeshi 2,500 huuawa kutoka pande zote na kwamba hilo linapaswa kusitishwa mara moja.
Soma pia:Marekani, Wahouthi waapa kuendelea kushambuliana
Kulingana na rais huyo wa Marekani, anatazamia kwa hamu mazungumzo hayo na Putin.
Katika jaribio la uwezo wake wa kufikia makubaliano, Trump anatumai kuwa anaweza sasa kumshawishi Putin pia kukubali kusitishwa kwa mapigano na kuruhusu hatua za kuelekea mpango wa amani wa muda mrefu ambao amedokeza unaweza kujumuisha makubaliano ya kimaeneo na Ukraine na udhibiti wa kiwanda cha nyuklia cha Zaporizhzhia.