MigogoroMashariki ya Kati
Trump atoa wito wa utoaji msaada zaidi wa chakula huko Gaza
30 Julai 2025Matangazo
Trump ameitoa kauli hiyo jana jioni akiwa kwenye ndege inayombeba rais wa Marekani ya Air Force One alipokuwa safarini akitokea Scotland, na akisisitiza kuwa mtu asiye na huruma au mwendawazimu ndiye asiyeweza kuguswa na madhila ya watoto wa Gaza.
Hayo yanajiri wakati ambapo Ujerumani na nchi kadhaa za Umoja wa Ulaya zimezuia pendekezo la kuiwekea Israel vikwazo kutokana na kuhusika kwake na hali mbaya ya kibinadamu inayoendelea kushuhudiwa katika Ukanda wa Gaza.