UchumiUlaya
Trump atishia kuweka ushuru wa ziada kwa bidhaa za EU
13 Machi 2025Matangazo
Tamko la Trump la kutaka kuongeza viwango vya ushuru kwa bidhaa za kutoka Umoja wa Ulaya linatishia kutanuwa vita ya kibiashara duniani, kutokana na mataifa hayo washirika wakubwa wa kibiashara wa Marekani kusema watachukuwa hatua za kulipa kisasi.
Trump amesema ikiwa Umoja wa Ulaya utaendelea na mpango wake wa kuongezea ushuru kwa baadhi ya bidhaa za Marekani mwezi Ujao,ataweka ushuru zaidi kwa bidhaa za mataifa hayo.
Soma pia:Ushuru uliotangazwa na Trump waanza kutekelezwa
Canada ambayo pia imeongezewa viwango vya ushuru na Marekani, tayari imeshajibu kwa kuweka ushuru mkubwa kwa bidhaa za kutoka Marekani.