Haki za binadamuMarekani
Rais Trump kuhudhuria ufunguzi wa "Alligator Alcatraz"
30 Juni 2025Matangazo
Trump ataandamana na Waziri wa Usalama wa Taifa Kristi Noem, aliyemtaka kuambatana naye, hii ikiwa ni kulingana na chanzo kinachofahamu suala hilo, ambacho hakikutaka kutambulishwa.
Takwimu za serikali zimeonyesha idadi ya wahamiaji kwenye kizuizi hicho imeongezeka hadi 56,000 kutoka 39,000 wakati Trump alipoingia madarakani.
Kituo hicho kilichoko kwenye eneo lenye idadi kubwa mamba na nyoka aina ya chatu kinafunguliwa wakati Trump, akitekeleza jitihada zake za kuzuia na kuwafurusha wahamiaji aliosema walioingia kwa wingi wakati wa utawala wa mtangulizi wake Joe Biden.